0

Mapokeo Matakatifu,Ndoa ya Bikira Maria haiwezi kutoshelezwa na maelezo kutoka kwenye Biblia.Inabidi kuwauliza wale walioishi naye ili tuweze kupata habari za maisha yake.Hapa ndipo umuhimu wa mapokeo Matakatifu unapoonekana.Kuhusu umuhimu wa Mapokeo Matakatifu(SomaYeremia6:16,Kumbukumbu la Torati32:1-12,Yohane20:30,Yohane21:25,Luka1:1-3 na 2Wathesalonike3:6-7).Ndugu zangu tusiyadharau Mapokeo Matakatifu ndio yaliyozaa Biblia.Kwa hiyo huwezi kuyahukumu Mapokeo Matakatifu kwa kutumia Biblia.Na Mapokeo Matakatifu ya Kanisa Katoliki yanaonesha Bikira Maria hakupata watoto wengine zaidi ya Yesu.

3.Matumizi ya jina Maria,Kuna wakina Maria chungu nzima kwenye Biblia.Kuna Maria wa Bethania(Yohane11:1-3),Maria mama yake Yohane,Huyu ndiye mama aliyempokea mtume Petro alipotoka gerezani(Matendo ya Mitume12:12),Maria Magdalena(Matayo28:1-8),Maria wa Roma(Warumi16:6),Maria mama yake Yakobo mdogo,Yose na Salome(Marko15:40),Maria Mama yake Yesu(Yohane19:25-27,Matendo ya Mitume1:14).Kwa hiyo ndugu zangu inabidi kujua yupi ni Maria mama yake Yesu ukilinganisha na wakina Maria wengine.Jina Maria limetafsiriwa kwa maana nyingi lakini maana inayokubalika na wengi ni "Kipenzi cha Mungu".Jina "Maria asili yake ni lugha ya "Kilatini",Miriam kwa"Kiebrania" na Mariam kwa "Kiaramayo".Majina haya yote yana maana sawa

Ndugu zangu aya za Biblia zinazoibua swali hilo ni(Matayo1:25,Marko6:1-6,Matayo12:46-50,na Luka8:19-21).Hizi aya ukizisoma zinataja kaka na dada za Yesu.Waweza kujiuliza hao kaka na dada za Yesu wanaotajwa kwenye aya hizo hapo juu ni kaka na dada zake wa damu?Ndugu yangu uliyeuliza hili swali,Ndoa ya Bikira Maria ilikuwa ya ajabu mno.Tunasema ilikuwa ya ajabu sababu alipata mimba pasipo tendo la ndoa.Maria akamwambia Malaika "Litakuwaje neno hili maana mimi sijui mume?Luka1:34).Bikira Maria alipata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.Kwa kuonesha Bikira Maria alipata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu soma Injili ya Luka1:35).Kanisa Katoliki linafundisha Bikira Maria hakuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu kwa kutumia hoja zifuatazo;1-Mila na desturi za Kiyahudi,Kwa Wayahudi suala la kuitana kaka na dada lilikuwa jambo la kawaida kama kwenye mila na tamaduni zetu za kiafrika.Mtu kumwita dada haina maana kwamba mlizaliwa tumbo moja.Au kumwita mtu fulani mama,baba au ndugu si lazima awe ndugu wa damu.Neno la Kigiriki"Adelphoi"kwa mwanaume na "Adelphai" kwa mwanamke.Maneno hayo yanaweza kutafsiriwa kama ndugu wa damu mfano kaka,dada,ndugu wa kambo mfano kaka au dada.Neno hilo laweza kutafsiriwa pia kama jamaa,jirani au rafiki.Kwa hiyo Biblia inapotaja ndugu au kaka na dada zake Yesu Kristo haina maana ya ndugu wa damu bali yaweza kuwa jirani,jamaa au rafiki.Waweza kurejea undugu wa Abrahamu na Lutu haukuwa undugu wa damu lakini wao wanaitana ndugu (soma Mwanzo13:8,Walawi10:4-5).



4-Wajibu wa watoto wa Kiisraeli,watoto wa Kiisraeli waliwajibika kuwatunza wazazi wao wanapozeeka au mmojawapo anapofariki.Kitendo cha Yesu kumkabidhi mama yake kwa mwanafunzi aliyempenda(Mtume Yohane) kinaonesha wazi kabisa Bikira Maria hakuwa na mtoto mwingine zaidi ya Yesu.Kama Bikira Maria angekuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu,Yesu mwenyewe asingethubutu kumkabidhi mama yake kwa mwanafunzi aliyempenda sababu ingetafsiriwa kama dharau kwa wadogo zake na kuwakosesha heshima katika jamii ya Kiisraeli sababu wao ndio walikuwa na wajibu wa kuwatunza wazazi wao.Hata katika tamaduni zetu za kiafrika,Baba akifariki watoto wanakuwa na wajibu wa kumtunza mama.Inasikitisha sana baba yako anafariki halafu mama yako unamkabidhi rafiki yako amtunze wakati wewe na wadogo zako mpo.Hii inaingia akilini kweli?wewe mwenyewe unayo majibu.Pia kama Bikira Maria angekuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu,Mbona msalabani hawakuonekana?Kitendo cha Yesu kumkabidhi mama yake kwa mwanafunzi aliyempenda ilionesha wazi kabisa hata mume wake Mtakatifu Yosefu alikuwa ameshafariki.Kama Yosefu ambaye ni baba mlishi wa Yesu angekuwa hai,Yesu asingethubutu kumdharirisha baba yake kwa kitendo cha kumkabidhi mama yake kwa mwanafunzi aliyempenda.Waweza kujiuliza kama Yosefu alikuwa ameshafiriki,Bikira Maria alizaa na nani?Na Yosefu angekuwa hai kipindi hicho tungemwona msalabani.Kwa hiyo ni hakika alikuwa ameshakufa (Yohane19:25-27).Kwa hoja hizo mnamo mwaka 553 huko Konstantinopoli,Mama Kanisa Mtakatifu sana alitangaza fundisho la kiimani(Dogma) kwamba,Bikira Maria mama wa Mungu(Theotokos) alikuwa Bikira kabla ya kumzaa Yesu(Ante partum-Kilatini),Alikuwa Bikira wakati wa kumzaa Yesu(In partum kwa Kilatini),na Alikuwa Bikira baada ya kumzaa Yesu (Post partum kwa kilatini).Kitendo cha Bikira Maria kumzaa Yesu hakikupunguza wala kuharibu ubikira wake bali kiliutakatifuza ubikira wake.(Rejea hati ya Mtaguso wa ll Vatican,Constitutio ya kidogma juu ya fumbo la Kanisa"Lumen Gentium No.53.Pia Jalimu la Maandiko Matakatifu(The Father of Biblical Science) Mtakatifu Jerome(437-420) alitafsiri Isaya7:14 kwa kutumia neno la Kiebrania"Alma" kuonesha kwamba Bikira Maria ni msichana ambaye ubikira wake umefichwa au wa siri.Ndio maana hata Kanisa Katoliki humwita Bikira Maria"Alma Mater" yaani Bikira aliye wa siri au aliyefichwa.Kwa hiyo Bikira Maria hakuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu.Kaka na dada wanaotajwa kwenye Biblia inawezekana kabisa walikuwa watoto wa akina Maria wengine lakini si Maria mama yake Yesu.

Chapisha Maoni

 
Top