Kati ya mataifa 192 yaliyofanyiwa uchunguzi na taarifa hiyo, 38 ni yale yaliyo katika hali ngumu zaidi, na kati ya hayo, kwenye mataifa 23 kuna mateso makali, 12 mateso kutoka katika serikali zao, na 11 kutoka kwa makundi ya kijeshi ya waasi, na 15 yapo katika hali ya manyanyaso na unyanyapaaji. Mataifa saba ni yale ambayo yapo katika hatari ya kunyimwa uhuru wa kuabudu, nayo ni Saudi Arabia, Iraq, Siria, Afghanistan, Somalia, Nigeria ya kaskazini na Korea ya kaskazini. Taarifa inalenga kurudisha matumaini kwa wanaoteswa, kupitia miradi ya Taasisi ya Kipapa kwa ajili ya makanisa hitaji.
Kardinali Mauro Piacenza, Mwenyekiti wa Taasisi ya Kipapa kwa ajili ya Makanisa hitaji amesema: uhuru wa kuabudu unapaswa kulindwa na kila utawala wa sheria, kwa namna ya pekee, mataifa ya kidemokrasia, na uhuru huo uonekane wazi hadharani.
Askofu Jacques Behnan Hindo, wa Madhehebu ya kikatoliki-siria, katika Hassake-nisibi, katoa ushuhuda kwamba, Sharia ya kiislamu inanyima uhuru wa dhamiri, na hivyo Siria hakuna uhuru wa kuabudu kwa wakristu, na hiyo ni kwa sababu, nchi ya Siria ni nchi iliyovamiwa, na uislam nchini humo ni siasa. Wadaeshi hawapingi wakristu peke yao, wanapinga yeyote asiye mdaeshi.
Katika taarifa hiyo, wamekumbukwa wanawake wawili ishara ya matumaini ya uhuru wa kuabudu: Asia Bibi, mpakistani aliyechini ya ulinzi mpaka sasa, na Ishrat Akhond, mbangladeshi aliyeuwawa katika shambulio la Dacca hivi karibuni.
Na Padre Celestine Nyanda
Related Posts
- MAPADRI HESHIMUNI SADAKA ZA WAAMINI12 Jan 2018Maoni
PAROKO wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeli jimboni Morogoro Padri Vivian Menezes, amewaasa mapadri nchini kushika njia ya utakatifu na kutham...Read more »
- WAZAZI WAWE MAKINI NA VIPINDI VYA LUNINGA KWA WATOTO12 Jan 2018Maoni
Na Angela Kibwana, Morogoro ASKOFU wa Jimbo Katoliki Morogoro Mhashamu Telesphor Mkude amewaonya baadhi ya wazazi wenye tabia ya kuwaacha watoto ...Read more »
- Maaskofu watoa ujumbe wa Kwaresima 20111 Feb 2018Maoni
MAASKOFU 35 wanaounda Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania wametoa ujumbe wa Kwaresima kwa 2018, huku wakiwataka waamini wakatoliki wote kuuitik...Read more »
- 20 Nov 2017Maoni
Tabia ya Baba Mtakatifu katika mawasiliano daima ni nyepesi, mtazamo na ishara zake ndiyo mtindo wake. Ni maneno ya Monsinyo Dario Vigano’ Mwenyek...Read more »
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni