Upendo usiomtambua Kristo kwamba amekuja katika mwili, akafanyika mwili, sio upendo ambao Mungu anawaamuru watu. Upendo wa namna hiyo ni upendo wa kidunia, wa kifalsafa, wa nadharia, upendo usio halisi, upendo laini laini. Upendo wa Mungu, ni upendo wa Neno aliyefanyika mwili. Anayefundisha upendo tofauti na huu, huyo atakuwa ni mpinga Kristo. Waamini wanapaswa kuishi na kuonesha upendo kama alivyofanya Kristo mwenyewe. Mafundisho haya ni sehemu ya mahubiri ya Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Misa Takatifu, kwenye Kikanisa cha Mt. Martha, kilichoko mjini Vatican, siku ya Ijumaa, tarehe 11 Novemba 2016.
Kanisa ni jumuiya iliyo katika uwepo wa Kristo aliyefanyika mwili. Yeyote anayekwenda kinyume na fundisho la umwilisho hawezi kuwa na upendo wa kweli, upendo wa dhati, upendo kama wa Kristo. Walio kinyume na upendo uliofanyika mwili, huishia kuishi maisha ya nadharia, bila uhalisia ndani yao. Baadhi ya wanaoamini hivyo, hujikuta wanaishia kwenye maigizo ya huzuni, maigizo ya Mungu bila Kristo, Kristo bila Kanisa, na Kanisa bila watu. Baba Mtakatifu Francisko, anawaalika waamini kuomba pamoja naye, ili kujihadhari na upendo nadharia, bali wajaliwe kuwa na upendo wa kweli, upendo unaoshuhudia huruma ya Mungu. Waamini wajifunze kutoka kwa Mt. Laurent aliyesema: maskini ni hazina ya kanisa. Alisema hivyo sababu maskini ni mwili wa Kristo unaoteseka. Hivyo ni muhimu kuishi upendo na kujali maskini.
Na Padre Celestine Nyanda
Idhaa ya Kiswahili, Radio Vatican.
Related Posts
- MAPADRI HESHIMUNI SADAKA ZA WAAMINI12 Jan 2018Maoni
PAROKO wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeli jimboni Morogoro Padri Vivian Menezes, amewaasa mapadri nchini kushika njia ya utakatifu na kutham...Read more »
- WAZAZI WAWE MAKINI NA VIPINDI VYA LUNINGA KWA WATOTO12 Jan 2018Maoni
Na Angela Kibwana, Morogoro ASKOFU wa Jimbo Katoliki Morogoro Mhashamu Telesphor Mkude amewaonya baadhi ya wazazi wenye tabia ya kuwaacha watoto ...Read more »
- Kwa msaada wa Roho Mtakatifu, Liturujia iwe ni shule ya sala!12 Jan 2018Maoni
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli. Huu ni ut...Read more »
- Papa Francisko: Wakristo ombeni zawadi ya upatanisho na umoja!01 Apr 2017Maoni
Maadhimisho ya Jubilei ya miaka 500 ya Mageuzi ya Kiluteri Duniani imekuwa ni fursa ya kujenga na kuimarisha Uekumene wa damu na huduma; maisha ya kir...Read more »
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni