“Mwanzoni
tulidhani hakutakuwa na kitu baada ya kukuta mchwa wengi lakini
tulipochimba zaidi tlishangaa kuiona mifupa yake, punje za rozari na
msalaba” Alisema Fr Francis Shawa ambaye yuko kwenye kamati ya mchakato
huu.
Kwa
sasa masalia hayo yamehifadhiwa katika kikanisa cha Askofu Mkuu
mwashamu Norbert Mtega wa jimbo kuu katoliki la Songea. Kwa sasa utaratibu unaofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu Songea wa kujenga mahali rasmi ili kuweka masalia ndani ya Kanisa.
Vilevile
baba alisema ya kwamba “Pamoja na sehemu hizo mbili yalipohifadhiwa
masalia hayo, itabidi tutengeneze upya kaburi lake pale Peramiho, ili
hapo pia pawe ni mahali maalum pa hija kwa watu binafsi wanaotaka
kuhiji. Hivyo, hija zitaweza kufanyika: Songea, Chipole, Peramiho na
Luwawazi-Likuyufusi, mahali alipozaliwa,”
Shime
shime marafiki pelekeni shida zenu;magonjwa, masomo,matatizo ya uzazi
na kadhalika kwa Mungu kupitia maombezi ya sista huyu ili aweze kuingia
katika orodha ya watakatifu. Pia tunaomba kuchangia mchakato huu kwa
akaunti ya jimbo la Songea ili kufanikisha mchakato huu ambao nighali
sana.
Katika upendo wa Kristu,
Chanzo cha habari http://bernadetambawala.blogspot.com/2012/04/masalia-ya-mwili-wa-sr-bernadeta.html
Vicenza-Marie
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni