Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi, tarehe 5 Novemba 2016 ameipongeza familia ya Asburg iliyokuwa inafanya hija ya kiroho mjini Roma, kama sehemu ya maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu. Baba Mtakatifu amefafanua kuhusu dhana ya familia katika mapana yake, kwa kugusia utajiri, tofauti na tunu msingi za maisha ya kifamilia ambazo, watu wanapaswa kuzigundua na kuzisimamia kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya familia ya binadamu!
Maadhimisho haya yanakwenda sanjari na kumbu kumbu ya Jubilei ya miaka 100 tangu Mwenyeheri Carlo wa Austria alipotawazwa kuwa Mfalme wa Austria. Uwepo wake wa kiroho miongoni mwao ni mwaliko wa kuyatazama yaliyopita kwa ari na moyo mkuu, ili kuweza kukabiliana na changamoto na mahitaji ya nyakati. Baba Mtakatifu anawashukuru na kuwapongeza baadhi ya wanafamilia hawa ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kujenga na kudumisha mshikamano na maendeleo ya binadamu kiutu na kitamaduni pamoja na kuendelea kusimama kidete kudumisha mradi wa Ulaya unaojikita katika tunu msingi za kiutu na Kikristo!
Baba Mtakatifu anawapongeza vijana wa kizazi kipya katika familia hii ya kifalme, ambamo kumeibuka pia miito mitakatifu ya kipadre na maisha ya kitawa. Baba Mtakatifu anamshukuru Mungu kwa kuiwezesha familia kuwa ni kitalu cha kwanza cha miito mitakatifu ndani ya Kanisa. Maisha ya ndoa ni wito mtakatifu unaopaswa kuendelezwa na kudumishwa. Mfalme Carlo wa Austria alikuwa ni Baba mwema wa familia, mtunzaji bora wa Injili ya uhai na amani. Ni kiongozi aliyeonja adha ya vita, alipopigana vita kama Askari wa kawaida, mwanzoni mwa Vita kuu ya kwanza ya dunia.
Kunako mwaka 1916, akiwa makini kwa Sauti ya Kinabii kutoka kwa Papa Benedikto wa kumi na tano, Mfalme Carlo, akasimama kidete kulinda na kutetea amani hata kama aligundua mwishoni kwamba, watu wengi hawakumwelewa na hivyo wakamdhihaki, lakini bado anaendelea kuwa ni mfano bora wa kuigwa na mwombezi mbele ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya amani duniani. Mwishoni, Baba Mtakatifu ameishukuru familia hii kwa kuihakikishia sala na sadaka yake katika safari ya maisha ya familia yao.
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.
Related Posts
- MAPADRI HESHIMUNI SADAKA ZA WAAMINI12 Jan 2018Maoni
PAROKO wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeli jimboni Morogoro Padri Vivian Menezes, amewaasa mapadri nchini kushika njia ya utakatifu na kutham...Read more »
- Kardinali Pengo: Jitahidini kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha12 Jan 2018Maoni
Yamekuwa ni mapokeo kwa Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam kutoa Daraja Takatifu ya Ushemasi kwa Majandokasisi wa ...Read more »
- Maaskofu watoa ujumbe wa Kwaresima 20111 Feb 2018Maoni
MAASKOFU 35 wanaounda Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania wametoa ujumbe wa Kwaresima kwa 2018, huku wakiwataka waamini wakatoliki wote kuuitik...Read more »
- WAZAZI WAWE MAKINI NA VIPINDI VYA LUNINGA KWA WATOTO12 Jan 2018Maoni
Na Angela Kibwana, Morogoro ASKOFU wa Jimbo Katoliki Morogoro Mhashamu Telesphor Mkude amewaonya baadhi ya wazazi wenye tabia ya kuwaacha watoto ...Read more »
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni