0
MT. RITA WA KASHIA
Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili Mavurunza Jimbo Kuu la Dar es Salaam inawatangazia waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuwa kutakuwa na Semina kwa Wanachamana wa zamani na wale wanaotaka kuwa Wanachama wa Chama cha Kitume cha Mt. Rita wa Kashia kuanzia tarehe 7 hadi 15 Mei, 2016 Parokiani Mavurunza. Semina itaanza saa 8:00 mchana hadi saa 12:00 jioni. 

Pia kutakuwa na uzinduzi wa Groto la Mt. Rita wa Kashia Parokiani Mavurunza siku ya sikukuu ya Mt. Rita tarehe 22 Mei 2016. Tarehe hiyo kutakuwa na baraka kwa watoto wadogo, baraka ya mawaridi, na baraka ya magari. Ibada ya uzinduzi wa Groto la Mt. Rita na kusimikwa kwa Wanachama wapya itaanza saa 9 Alasiri. Wote Mnakaribishwa.

Chapisha Maoni

 
Top